Kamanda Shanna ametoa hadhari hiyo baada ya kutokea ajali na kusababisha vifo vya watu 3 . Ajali hiyo iliyotokea majira ya saa 9 mchana katika kijiji cha Msolwa, wilaya ya kipolisi Chalinze, ilihusisha gari la Serikali, chini ya wizara ya Viwanda,Biashara na Uwekezaji, yenye namba za usajili STK 923 aina ya TOYOTA-LAND CRUISER , iliyokua ikiendeshwa na Bw. Peter mwenye umri wa miaka 23, mkaazi wa Mkoa wa Dar Es Salaam .
Chanzo cha ajali hiyo, kinaelezwa kua ni uzembe wa Dereva aliyekua anaendesha gari ya Serikali, alipohama upande wake wakati akiyapita magari mengine kwa mwendokasi bila kuchukua tahadhari na kuligonga gari lenye namba za usajili T 920 AQV aina ya SCANIA , ambayo dereva wake alitoroka mara tu baada ya ajali .
