Waziri Nchemba amelitaka jeshi la polisi kuchunguza kwa kina tukio hilo ili kumbaini askari aliyehusika na hilo na kuwaambia wananchi nini kinachoendelea.
“Kama Waziri mwenye dhamana nalaani vikali sana tukio la kupoteza maisha ya binti wetu ambaye hakua na hatia, matukio ya namna hii naona yanaanza kujirudia tena kwa kasi matukio ya kupoteza maisha kwa watu wasiokuwa na hatia hasahasa katika masuala yanayohusu siasa ni mambo ambayo hayakubaliki na ninalaani kwa nguvu zote. . Alisema Waziri Mwigulu,“amesema Waziri Nchemba
Ameongeza kwa kusema kuwa amemuelekeza IGP mara baada ya tukio kutokea wafuatilie na wachunguze kubaini wote waliosababisha tukio hilo na kuweza kuwafikisha katika mikono ya sheria ili sheria ichukue mkondo wake.
Dkt. Mwigulu amewataka wananchi wote kuepuka vitendo hivi vinavyoweza kusababisha madhara kwa namna moja au nyingine na wanapoona matukio ya namna hii watoe ushilikiano kwa vyombo vya ulinzi na usalama ili wausika wafikishwe katika vyombo vya usalama.
