Auawa kwa kisu wakati akimtetea mpenzi wake

Mwanaume mmoja mwenye umri wa makamo chini Kenya katika eneo la Tudor Mombasa, ameuawa kwa kuchomwa na visu akijaribu kuwasuluhisha wapenzi waliokuwa wakigombana nyumbani kwao.

Kwa mujibu wa mjumbe wa nyumba 10 wa eneo hilo Benson Okello. Marehemu alichomwa visu mara kadhaa baada ya kujaribu kumuokoa mwanamke mmoja mwenye umri wa miaka 25 aliyekuwa akipigwa na mume wake, akimtuhumu kutumia dawa za kupanga uzazi ili asimzalie mtoto.

Okello amesema tukio hilo limewaacha pia wenza hao wakiwa wamejeruhiana vibaya na kupelekea kukimbizwa hospitali, ambako wamelazwa katika vyumba vya wagonjwa mahututi.

Kwa mujibu wa majirani wamesema wawili hao wamekuwa watu wa kugombana mara kwa mara, kwa sababu hiyo hiyo ya kutumia njia za uzazi wa mpango.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo