Mwalimu achapwa viboko na mwalimu mwenzake kwa kuchelewa shule


 Mwalimu katika Kaunti ya Nyamira nchini Kenya amelazwa katika hospitali ya Ikonge baada ya kushambuliwa na mwalimu mkuu kwa madai ya kuchelewa kufika shuleni.


Mwalimu huyo wa Sekondari aitwaye Vincent Onyancha amesema alifanyiwa vurugu mbele ya wanafunzi wake darasani wakati akifundisha ambapo mkuu huyo alimpiga makofi na kumpiga mateke kisha kumburuza hadi ofisini kwake ambako aliendelea kumpiga.


Maafisa wa Chama cha Walimu wa Shule za Sekondari (KUPPET) wamelaani tukio hilo na kuitaka Tume ya Huduma kwa Walimu (TSC) kuchukua hatua za kisheria dhidi ya mwalimu mkuu huyo. Hata hivyo TSC imesema imeanza kufanya uchunguzi.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo