Uongozi wa kijiji cha
Ilindiwe kwa kushirikiana na wa Kata ya Mang'oto wilayani Makete mkoani Njombe
wanafanya uchunguzi wa sababu zilizopelekea mwanafunzi mmoja kufeli mtihani wa
kuhitimu darasa la 7 licha ya mwanafunzi huyo kuwa na uwezo wa kielimu darasani
Akizungumza katika
mahafali ya darasa la 7 yaliyofanyika leo Novemba 11, 2017 katika shule ya Msingi Ilindiwe, Mwalimu Mkuu wa shule
hiyo Bw. Faustin Ntakunga amesema katika mtihani wa mwaka huu wamehitimu
wanafunzi 6 ambapo kati ya hao mmoja ndiye aliyefeli na kusema wanalazimika
kuchunguza kujua sababu za mwanafunzi huyo kufeli ilihali alikuwa na uelewa
mkubwa darasani
Mbali na hilo uongozi
wa shule hiyo umewakabidhi wanafunzi hao kwa wazazi pamoja na uongozi wa
kijiji, ambapo wamepokelewa na Mwenyekiti wa kijiji Bw Yosofati Idawa na Afisa
Mtendaji wa Kijiji Victor Mapunda
Akizungumza katika
mahafali hayo, Afisa mtendaji wa Kata ya Mang'oto Bw. Mengi Chalamila
amewasisitiza wazazi uhakikisha wanafunzi hao wanawapeleka shuleni ili
kuepukana na mkono wa sheria endapo hawatafanya hivyo
Kwa upande wake mgeni
rasmi katika mahafali hayo ambaye pia ni Diwani wa kata ya Mang'oto Mh Osmund
Idawa amesema atahakikisha uchunguzi unafanywa kujua sababu za mwanafunzi huyo
mmoja kufeli, na endapo itaonekana kulikuwa na shinikizo la mwanafunzi huyo
kuambiwa afeli, hatua za kisheria zitachukuliwa kwa mhusika
Jumla ya wanafunzi 6
wamehitimu elimu ya msingi katika shule hiyo ya Msingi Ilindiwe mwaka huu, huku
wanafunzi watano wakifaulu na mmoja kufeli
