Live kutoka Bandarini: Mtu asiyejulikana amchefua Rais Magufuli


Rais Dkt John Magufuli amefanya ziara ya kushtukiza katika bandari ya Dar Es Salaam hii leo na moja ya jambo lililomsikitisha ni kukuta magari ya wagonjwa yaliyoagizwa na mtu asiyejulikana na kuwepo bandarini hapo tangu 2015 bila mwenye nayo kujulikana

Kwa Mujibu wa taarifa zinazotolewa mbele yake sasa hivi na maafisa wa bandari magari hayo yamefika bandarini hapo tangu 2015 Juni na taarifa zikionesha magari hayo yaliagizwa na ofisi ya Rais taarifa ambazo zinaonesha utata

Rais Magufuli amewauliza viongozi mbalimbali lakini bado wameonesha kuyumbishwa kwa kuwa taarifa hizo hazimridhishi

Ametoa siku saba kuanzia leo uchunguzi ufanywe na vyombo vya usalama wamwambie ni mzigo wa nani na hayo magari yameletwa na wakina nani

Pia amechukizwa na mawaziri wa wizara husika kutofahamu kuhusu walioagiza hayo magari

Kwa nini Waziri Hukujua, kwa nini IGP hukujua, kwanini PCCB hukujua, je kwa nini Mimi nijue? amesema Rais Magufuli


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo