Watoto yatima waliopo kituoni hapo
Mkuu wa wilaya ya Makete Josephine Matiro (kushoto) akiwa amembeba mtoto yatima anaelelewa kwenye kituo hicho
Castoel Obadia akisoma risala
Mkuu wa wilaya ya Makete (kushoto) akiagana na Sista Anna ambaye ni mwanzilishi wa kituo hicho
Diwani wa kata ya Bulongwa Ericka Sanga akiagana na sister Anna
Moja ya jengo la kituo hicho
Na Edwin Moshi, Makete
Jamii imeshauriwa kuona
umuhimu wa kutembelea watoto yatima wanaolelewa katika vituo mbalimbali kwani
kwa kufanya hivyo kutasaidia wao kujiona wanathaminiwa na kupendwa kama watoto wengine
Hayo yamesemwa na mkuu wa
wilaya ya Makete Mh. Josephine Matiro wakati alipotembelea kituo cha watoto
yatima cha Bulongwa Orphans Home kilichopo kata ya Bulongwa wilayani Makete
ambapo pamoja na mambo mengine ametoa msaada wa vitu mbalimbali kwa ajili ya
watoto hao
Mh. Matiro amesema watoto yatima
wanahitaji faraja ya hali ya juu kutoka kwa wanajamii hivyo wanapotembelewa na
watu mbalimbali hujisikia faraja na kufanya maisha yao kuwa ya furaha zaidi
Amesema ameona ni vyema
kuwaona watoto hao wanaolelewa kwenye kituo hicho na kutoa msaada kidogo kwa
ajili ya watoto hao ili wafurahie sikukuu zilizopo mbele yao
kama watoto wengine wanaoishi na wazazi ama
walezi wao majumbani
“Nimeona si vyema kula sikukuu
mimi kabla ya hawa watoto nimeleta hiki kidogo kwa ajili ya watoto hawa wao
waanze kusherekea mapema kwa kuwa jukumu la kuwalinda watoto hawa ni letu sote,
na mimi kama mkuu wa wilaya binafsi, nimeguswa
na ndio maana nimekuja kuwaona” alisema Matiro
Katika hatua nyingine mkuu
huyo amefurahishwa na jinsi watoto hao wanavyotunzwa na kulelewa katika maadili
mema, huku akisisitiza kituo hicho kuendelea na moyo huo wa kuwalea watoto hao
katika maadili mema
Akisoma risala kwa mkuu wa
wilaya moja ya mtumishi wa kituo hicho aliyejitambulisha kwa jina la Castoel
Obadia amesema kituo hicho kinaendeshwa kwa kutegemea misaada kutoka nje pamoja
na ndani ya nchi, lakini kwa kiasi kikubwa ni kutoka kwa Sister Anna ambaye
ndiye muanzilishi wa kituo hicho
Amesema mafanikio yaliyopo
katika kituo hicho kuwa ni pamoja na kuanzisha miradi mbalimbali ikiwemo nyumba
ya kulala wageni, mashine ya kusaga na kukoboa mahindi, mashine ya kukamulia
alizeti pamoja na mradi wa ng’ombe nguruwe na mbuzi ambayo kwa kiasi Fulani
huwaingizia kipato inagawa hakitoshi kulingana na mahitaji ya kituo hicho
Amezitaja changamoto
zinazokikumba kituo hicho kuwa ni pamoja na uhaba wa fedha za kuwalea watoto
hao pamoja na wafanyakazi, uhaba wa maji,kuiomba halmashauri ya wilaya ya
Makete kusamehe kutoza kodi kwenye miradi ya kituo hicho,pamoja na ukosefu wa
nyumba za watumishi
Wamesema kwa kuwa mahitaji ya
kituo hicho ni makubwa ukilinganisha na kipato hivyo wameona ni bora kuanzisha
miradi hiyo kama njia ya kujiongezea kipato
lakini wanaiomba halmashauri iwasamehe kodi ili fedha hizo zitumike kwenye
kituo hicho
Mkuu wa wilaya ameahidi
kuzishughulikia changamoto hizo kwa kushirikiana na viongozi wengine ili kituo
hicho kizidi kutoa huduma ya kulelea watoto yatima
Katika ziara hiyo mkuu wa
wilaya aliambatana na diwani wa kata ya Bulongwa Mh. Erica Sanga ambaye
amemshukuru mkuu wa wilaya kwa moyo wake wa kutembelea kituo hicho
Kituo hicho kinapokea na kulea
watoto waliofiwa na mama yao
na kuendelea kuwatunza hadi pale wanapokuwa tayari kujitegemea kwa kuwa wengi
hupenda kuishi hapo hata wakienda kusoma katika shule mbalimbali