Rais Magufuli amponda Kubenea, Amsifia Prof. Kitila Mkumbo

RAIS Dkt John Magufuli ameshangazwa na kitendo cha mbunge wa Ubungo (CHADEMA) Saed Kubenea kushindwa kwenye tukio la kuzinduliwa kwa hosteli za kisasa za Chuo kikuu cha Dar Es Salaam hii leo

Rais Magufuli amesema ameamua kumuita mbunge huyo kusema au kuomba lolote kutoka kwa Rais na yeye angempatia, lakini kwa kuwa hayupo, wananchi wampelekee shida zao na yeye alizepeke serikalini ili zifanyiwe kazi

Amesema wakati wa kampeni mbunge huyo aliahidi vitu vingi hivyo anatakiwa kushirikiana na serikali kuvitekeleza

Katika hatua nyingine amemsifia katibu mkuu wa wizara ya Maji Prof Kitila Mkumbo na kusema ni mtu safi, na yeye hateui VILAZA

Rais Amesema atamshangaa katibu mkuu huyo endapo chuo kikuu cha DSM kitakosa maji wakati yeye ni mwana jumuia ya chuo kikuu, na pia ameteuliwa kuwa katibu mkuu wa wizara ya maji na umwagiliaji

Amesema Prof Kitila alipoteuliwa kuwa katibu mkuu, alikwenda ofisi za CCM kutafuta na kuisoma ilani ya uchaguzi ya chama hicho ya 2015-2020 na kutafuta kipengele cha Maji ili aanze utekelezaji wa ilani hiyo


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo