Askofu awavaa Gwajima na Bashite, adai wanajuana

Na MatukiodaimaBlog 

ASKOFU  (mstaafu)  wa kanisa la  kiinjili la  Kilutheri  Tanzania (KKKT)  dayosisi ya  Iringa Dkt. Owdenburg Mdegella amesema   watanzania  wana mambo mengi ya  kufanya  ikiwa  ni pamoja na kujikita katika shughuli za  kiuchumi badala ya kupoteza muda  mwingi  kujadili  mambo  ya  Daud Bashite.

Akitoa  salama  za Pasaka  jana katika  usharika  wa kanisa kuu Dkt  Mdegella  alisema kuwa  watanzania wanapoteza  muda  mwingi kwa jambo hilo badala ya  kushughulika na mambo ya msingi yenye  tija kwa  Taifa .

“ Watanzania  wiki  tatu tunapoteza  muda kwa  habari za Bashite na Gwajima …hawa  wote  wametoka Mwanza wanajuana  vizuri nawaombeni  watanzania  tusipoteze  muda bure  tujikite kwenye mambo ya  kiuchumi  mtu kama amedandia  vyeti  atakamatwa  kwa  utaratibu  sasa  sisi  tumebaki  Bashite   Bashite yaani  ukitaka  kujua  nchi  hii watu  wanapenda majungu angalia walivyokomalia hii la Bashite “

Alisema  Dkt  Mdegela  kuwa  watu  wanapoteza  muda  kushinda vijiweni  kuzungumia Bashite  badala ya  kwenda kutafuta shughuli  za  kiuchumi kwa  ajili ya kupata fedha  .

Katika  hatua  nyingine  Dkt  Mdegella alipongeza kazi  nzuri  inayofanywa na Dayosisi    hiyo  chini ya  askofu mteule Blaston  Gavile kuwa heshima  kubwa  aliyoionyesha  kwa yeye kama askofu aliyeongoza kanisa hilo kwa  miaka 30 ya  kustaafu imekuwa ni  heshima  kubwa kwa kanisa  hilo ila mrithi  wake  anafanya  kazi  aliyomuachia vizuri sana.

Hivyo  alishauri kanisa  hilo  kuanzisha baraza  la  wazee washauri nay eye  atakuwa  mwenyekiti wa  washauri  hao ili  kulifanya kanisa   hilo  kuendelea  kufanya mazuri   zaidi.

Kwa  upande  wake askofu Mteule  wa  Dayosisi ya  Iringa katika  salam  zake  aliwataka  waumini  wa kanisa  hilo kuendelea  kuuombea  mkoa  wa Iringa  na maeneo  mbali  mbali kuachana na matukio ya  ubakaji na ulawiti ambayo yanazidi kuongezeka  siku hadi  siku .

“ Salam  zangu  kwenu  waumini ni  kuendelea  kuomba kwa ajili ya Taifa na mkoa wa Iringa tusema Mungu yatosha kuendelea  kusikia matukio ya ajabu ndani ya Taifa  letu …tuendelee  kuiombea nchi  yetu  kuwa ni ya amani  na kuepuka matukio yote ya utekaji na mauwaji kwenye    hili Taifa “

Alisema  Kanisa  limesikitishwa  sana  na mauwaji ya  askari  nane  waliouwawa  kinyama kwa  risasi na  kuwa kazi ya  wakristo isiwe  ya  kulalamika mitaani  kama  ilivyo kwa mataifa   kazi kubwa  iwe  ya  kufunga na kuomba kwa ajili ya taifa .


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo