Wafugaji watakaoingiza mifugo yao kwa Wakulima kuchapwa Viboko 70

Viongozi wa mila kutoka jamii ya kifugaji katika kijiji cha Naberera wilaya ya Simanjiro wameanza kutekeleza adhabu ya kuchapa bakora sabini kwa wafugaji wanaoingiza mifugo kwenye mashamba ya wakulima na kuharibu mazao ili kukomesha tabia hiyo inayochangia kuongezeka kwa migogoro kati ya wakulima na wafugaji kwenye kijiji hicho. 

Wakizungumza na vijana wa jamii ya kifugaji wazee na viongozi wa mila wamesema wamefika hatua hiyo baada ya kuongezeka kwa migogoro kati ya wakulima na wafugaji inayotokana na tabia ya baadhi ya wafugaji kutofuata taratibu.

Baadhi ya watendaji wa serikali kata ya Naberera wamesema tabia hiyo imeleta madhara kwa jamii hizo mbili lakini tayari wameunda kamati ya kuondoa migogoro hiyo.

Mwenyekiti wa kijiji cha Naberera Jacob Korosi ametumia nafasi hiyo kuwaonya wafugaji kuacha tabia hiyo kwakuwa watanzania wana haki sawa kwenye ardhi bila kujali anatoka jamii gani.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo