Uongozi wa Young Africans Sports Club umekanusha habari ambazo zimekuwa zikisambazwa zikisema Mwenyekiti wa Young Africans Sports Club amejiuzulu wadhifa huo.
Katika taarifa uliyoitoa uongozi wa Yanga umesema unasikitishwa na habari hizo na unawaomba wanachama wote kuupuzia ujumbe huo wenye malengo ya upotoshaji, pia unazidi kuwakumbusha wanachama kuwa habari sahihi zinatolewa na uongozi huo na si vinginevyo! Bw Yusuf Mehbob Manji bado ni Mwenyekiti wa Young Africans Sports Club!
Imetolewa na Uongozi wa Young Africans Sports Club Daima Mbele Nyuma Mwiko!
JIUNGE NA EDMO BLOG SASA
Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube