Inasikitisha: Kijana wa Miaka 20 afariki Dunia Baada ya Kunywa Viroba 14 wiayani Makete

Vitendo vya unywaji pombe kupita kiasi vimeendelea kuleta madhara wilayani Makete mkoani Njombe baada ya kijana Edward Sanga (20) kufariki dunia kutokana na kunywa pombe kupita kiasi

Kwa mujibu wa taarifa za mashuhuda zinasema kuwa tukio hilo la unywaji pombe kupita kiasi limetokea jana Usiku katika kijiji cha Lupalilo Wilayani hapa baada ya kijana huyo aliyekuwa na rafiki yake kunywa pakiti 14 za pombe aina ya Valuu na kuondoka kilabuni hapo ndipo leo asubuhi kukutwa maeneo ya kilabuni hapo akiwa Amefariki dunia

Bi Bertha Henigen Ni Afisa mtendaji wa kata ya Lupalilo anazungumzia namna tukio hilo lilivyotokea Kwa kusema kiwango kikubwa cha pombe alichokunywa ndicho kimepelekea kifo cha kijana huyo

Muhudumu wa kilabu alipokuwa akinywa pombe marehemu kabla umauti kumfika Bi Juliana Sanga amesema ni kweli alikuwa akinywa pombe kilabuni hapo na baadaye kuungana na rafiki yake ambaye alimnunulia pombe hizo


Mmiliki wa Kilabu cha pombe alipokuwa akinywa pombe marehemu kabla ya kupoteza maisha Bw. Chesko Sanga amezungumzia tukio hilo pamoja na diwani wa kata hiyo Mh Imani Mahenge ambaye amesema kata yake imempoteza kijana aliyekuwa tegemeo katika shughuli za maendeleo kijijini hapo huku pia akitoa onyo kwa vijana wenye tabia kama hiyo kuacha kupoteza muda wao kunywa pombe kupita kiasi na badala yake wajikite kujenga nchi kupitika shughuli mbalimbali zilizohalalishwa na sheria za nchi


Baba Mdogo wa marehemu akizungumza na mwandishi wetu amesema wamekuwa wakimuonya kijana wao kuhusu unywaji wa pombe kali ambazo alikuwa akinywa kwa kujificha bila wao kujua ingawa jitihada zao kama familia hazikuzaa matunda


Jeshi la polisi lilifika eneo la tukio na kuukagua mwili wa marehemu ambao haukukutwa na jeraha lolote na kugundulika kuwa kifo cha marehemu kimetokana na kunywa pombe kali maarufu kama viroba kupita kiasi, na kuruhusu familia kwenda kuzika mwili huo, huku wakisisitiza Wamiliki kuzingatia muda wa kufunga vilabu vya pombe uliowekwa kisheria


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo