AFISA wa polisi wa kikosi cha Recce mapema Ijumaa alifikishwa
mbele ya mahakama ya Nyeri Kenya kushtakiwa na kosa la kupoteza bunduki
yake.
Bw Mike Mutwiri Mbuba alishtakiwa kuwa mnamo usiku wa
Julai 13-14, 2016 akiwa katika kambi ya mafunzo ya polisi wa Recce iliyo
Solio Ranch eneobunge la Kieni, Kaunti ya Nyeri, kinyume na sheria
aliacha bunduki yake chini ya godoro jambo ambalo lilisababisha bunduki
hiyo kupotea.
Bw Mbuba hata hivyo alikana makosa hayo mbele ya Hakimu Mkazi Onesmus Towet.
Aliachiliwa kwa dhamana ya Sh50,000 au pesa taslimu Sh40,000.
Upande wa Mashtaka ulisema wako na polisi saba watakaotoa ushahidi kuhusiana na kisa hicho.
