Mwanamuziki
wa Kimataifa wa Miondoko ya Dansi kutoka Nchini Congo, Antoine
Christophe Agbepa Mumba maarufu kama "Koffi Olomide" amehukumiwa kifungo
cha miezi 18 jela baada ya kuonekana na hatia ya kumdhalilisha kwa
kumpiga dansa wake wakati wakiwasili kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa
wa Jomo Kenyatta Nchini Kenya hivi karibini.
Mwanamuziki
huyo alikamatwa mapema leo akiwa nyumbani kwake katika mji wa Kinshasa
na kupelekwa Mahakamani moja kwa moja na kukutwa na hatia hiyo.
Hukumu
hiyo imetolewa baada ya ushahidi huo kuonekana akimpiga dansa wake na
atatakiwa kuitumikia adhabu hiyo kwani hajapewa nafasi ya kulipa faini
ya aina yoyote ile.
hatua
ya kumkamata Mwanamuziki huyo ilifikiwa baada ya kuanzishwa kwa kampeni
ya baadhi ya wadau wa maswala ya kijamii wakiongozwa na Zakarie
Bababaswe aliyefungua kesi kwa niaba ya Serikali ikiwa ni madai ya
udhalilishaji kwa dansa wake, na Mwanasheria Mkuu wa Serikali ya Kongo,
kuamua kukamatwa kwake na kusema anataka haki itendeke.
CHINI NI VIDEO INAYOONYESHA TUKIO HILO.
CHINI NI VIDEO INAYOONYESHA TUKIO HILO.
