Wanyama hawa "wammaliza" Mkuu wa Mkoa wa Njombe akiwa Makete kikazi

Hivi karibuni Mkuu wa mkoa wa Njombe alifanya ziara wilayani Makete kukagua utekelezaji wa mradi wa TASAF awamu ya tatu kwa wanufaika katika vijiji kadhaa wilayani hapa

Mnyama anayeonekana kwenye picha hapo juu ni maarufu kwa jina la SIMBILISI na asilimia 90 ya wanufaika wa TASAF wamesema kuwa wanafuga wanyama hawa ambao wanazaliana kwa kasi, unakuta mtu alinunua wawili lakini ndani ya muda mfupi akajikuta anao zaidi ya kumi

Hali hiyo ilimvutia mkuu wa mkoa wa Njombe Dkt Rehema Nchimbi na kuhamasisha wanancho wa makete wawafuge wanyama hawa na wilaya itafute soko la kuwauza kwa kuwa watahitajika sana hasa uwekezaji wa madini ya Mchuchuma na Liganga yaliyoko Ludewa ukianza wanyama hao watahitajika sana


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo