Na JONATHAN MANYINDO.
MWANAMUME aliyepatikana na hatia ya kushiriki ngono na mbuzi amehukumiwa kifungo cha miaka 14 jela na mahakama Taita Taveta Kenya.
James Mbithe
alishtakiwa kuwa mnamo Julai 9 katika kijiji cha Mgeno alifanya mapenzi
na mbuzi anayemilikiwa na Bi Hannah Mambori.
Upande wa
mashtaka ukiongozwa na Inspekta Peter Milimo ulisema mshukiwa
alifumaniwa na mlalamishi aliyekuwa ameenda kuwaangalia mbuzi wake 12
waliokuwa machungani mita 300 kutoka nyumbani kwake.
Alimpata mshukiwa aliyemfahamu vyema akiwa amevua suruali ndefu yake huku mbuzi akitokwa na damu.
Baadaye
aliripoti kisa hicho kwa mzee wa kijiji na baadaye kwa afisa wa matibabu
ya mifugo ambaye alithibitisha kwamba mnyama huyo alikuwa amechafuliwa.
Mshtakiwa
anadaiwa kumtendea mbuzi huyo kitendo hicho mchana kama adhabu baada
yake kuingia shamba lake la mahindi na kuharibu mimea.
Mshtakiwa alikiri kosa hilo akisema hangeweza kukanusha kwa kuwa ulikuwa ndio ukweli.
Akijitetea, Mbithe, 59, aliomba ahurumiwe akisema ni mzee na kwamba alihadaiwa na shetani.
Akitoa
hukumu, Kaimu Hakimu Mkuu Wundanyi Bi M. Chesang alisema kwa kuzingatia
kujitetea kwa mshtakiwa, ripoti ya hali ya kiakili kutoka kwa Afisi ya
Uchunguzi wa Hali za Kiakili, na sheria, mshtakiwa anafaa kutumikia
kifungo cha miaka 14 jela.
Kampeni
Hukumu hiyo
imetolewa chini ya wiki moja baada ya Idara ya Mahakama, katika kaunti
ndogo ya Taita kuzindua kampeni dhidi ya dhuluma za kimapenzi.
Hii ni baada
ya polisi kusema asilimia 12 ya visa vya uhalifu vilivyoripotiwa kutoka
eneo hilo kipindi cha miezi mitatu ni za dhuluma za kimapenzi.