Rungu jingine lililoshushwa na serikali kwenda MSD

Mkurugenzi wa Bohari ya Dawa (MSD), Cosmas Mwaifwani ameagizwa na Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya, Dkt. Donan Mmbando kwa niaba ya Rais, kuhakikisha kuwa dawa zote za Serikali zinakuwa na utambulisho maalum ili endapo zitakutwa katika maduka ya dawa binafsi, hatua za kisheria zichukuliwe dhidi ya wamiliki wa maduka hayo.

MSD inahudumia hospitali za Serikali tu na vituo vyake na kamwe dawa ambazo husambazwa na MSD hazipaswi kuuzwa kwa wamiliki wa maduka ya dawa binafsi. Hili ni katazo la kisheria, hivyo ni kosa la jinai kwa dawa za Serikali kukutwa kwa wamiliki wa maduka ya dawa binafsi. 

Mkurugenzi huyo alikiri kuwa ni kweli wapo watumishi wasio waaminifi ambao wamekuwa wakiiba dawa hizo.

Aidha, Mkurugenzi huyo aliongezea kuwa, MSD itafungua maduka ya dawa makubwa karibu na mahospitali ya Serikali ili kurahisisha zaidi upatikanaji wa madawa kwa urahisi ikiwa ni sambamba na kusambaza madawa hayo kote nchini katika vituo vya afya kwa wakati, ili wananchi wote wenye uhitaji wa madawa waweze kupata bila tabu yoyote ile.

Mkurugenzi huyo ametoa namba maalumu ya simu, ambayo haitatozwa gharama (bure) itakayobandikwa kwenye vituo vya afya na mahospitali yote ya serikali kwa dhumuni la kumwezesha mwananchi kutoa taarifa MSD endapo atapata taabu kupatiwa dawa.  


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright 2025 EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo