Hili ndio Basi la Singida United walilolitambulisha leo

 Klabu ya Singida United imetambulisha ramsi basi lake jipya itakalotumia kwa msimu ujao wa Ligi Kuu Bara.

Basi hilo lenye thamani ya Sh 350 milioni limezinduliwa rasmi na litaanza kutumika katika safari za timu hiyo iliyopanda daraja msimu huu.

Katika basi hiyo, Singida imeweka picha za Rais wa timu hiyo, Mwingulu Nchemba ambaye ni Waziri wa Mambo ya Ndani pamoja na picha ya mmiliki wa timu, Yusuf Mwandami.

Ofisa Habari wa timu hiyo, Festo Sanga alisema wataanza maandalizi yao hivi karibuni ili kujiandaa na msimu mpya wa Ligi Kuu huku wakitarajia kukamilisha usajili wa nyota wachache waliosalia.

Meneja wa klabu ya Singida United Festo Sanga akizungumza na waandishi wa habari wakati wa kulitambulisha basi lao jipya litakalotumika kwa safari za ndani za timu ya Singida United.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright 2025 EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo