Wananchi waishio karibu na mto Ruvu wachukua maamuzi magumu

Wananchi wa vijiji vya Kituri na Kifaru wilayani Mwanga mkoani Kilimanjaro wamelazimika kuchukua hatua za kusafisha mto Ruvu  kwa kuondoa Magugu maji,magogo na tope kwa kutumia Ngalawa na Trekta  ili kunusuru mto huo ambao uko hatarini kukauka.

Akizungumza wakati wa zoezi la kusafisha mto huo mkurugenzi wa shirika la mazingira na utalii Tanzania (TETEO) Bw.Ally Makiade  amesema hali ya mto huo kwa sasa ni mbaya kutokana na kushamiri kwa vitendo vya uharibifu wa Mazingira 

Amesema zoezi la kuondoa uchafu katika mto huo ni gumu kutokana na ukosefu wa vifaa kwa madai kuwa kuna magogo makumbwa ambayo yanahitaji katapila na kwamba  zoezi hilo litasaidia kwa kiasi kikubwa kunusu mto huo ambao unategemewa kwa kiasi kikubwa na wananchi wa wilaya hiyo.
 
Kwa upande wake mhandisi wa mazingira anayesimamia raslimalii za maji kutoka bonde la pangani Bi.Arafa Majid amewataka wadau mbalimbali kujitolea kusafisha mto huo kwa kuwa maji mengi yanapotea kutokana na mto huo kujaa uchafu na magugu maji ambayo kama hayataondolewa mapema kuna hatari ya maji kukauka kabisa.
 
Baadhi ya wananchi wa wilaya ya Mwanga ambao wamejitokeza kusafisha mto huo wamesema hali ya mto huo kwa sasa ni mbaya kutokana na maji kuanza kupungua kwa kasi ikilinganisha na miaka kumi iliyopita na kwamba wananchi wa wilaya hiyo wanategemea maji ya mto huo kwa  ajili ya matumizi ya nyumbani na umwagiliaji.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo