Wananchi wa kijiji cha Makusi wilayani Makete wajianzishia utaratibu wao wa kuuza bidhaa

Wananchi na wafanyabiashara wa kijiji cha Makusi kata ya Itundu wilayani Makete mkoani Njombe wameulalamikia uongozi wa kata hiyo kuahidi kujenga soko lakini ahadi hiyo haijatimia

Wakizungumza na mwandishi wa eddy blog baadhi ya wananchi waliojitambulisha kwa majina ya Christina Mbwilo na Sayuni Mbilinyi wamesema kuwa kijiji hicho hakina soko la kudumu kwa muda mrefu ambapo watu hufanya biashara sehemu yeyote

Wamesema kwa sasa soko linalotumika kwa muda halina vyoo hali inayopelekea watumiaji wa soko hilo kujisaidia kwenye vyoo vya nyumba za majirani wa soko hilo hali inayosababisha kero kwa majirani hao

Mwenyekiti wa kijiji hicho Bw. Yohana Msigwa amesema uongozi wa kata ya Itundu umeliweka suala la ujenzi wa soko katika mikakati ya kata hivyo amewataka wananchi kuwa na subira

Amesema kwa sasa wamefyatua tofali 3000 kwa ajili ya ujenzi wa nyumba za walimu wa shule za msingi katika kata hiyo hivyo ujenzi huo ukikamilika watashughulikia ujenzi wa soko

Naye afisa mtendaji wa kata ya Itundu Bw Isaack Chengula amekiri kuwepo kwa chagamoto hiyo na kusema kuwa wanasubiri uchaguzi wa Oktoba 25 mwaka huu ukikamilika, watampata diwani ambaye watashirikiana pamoja kutatua chagamoto hiyo


Amewataka wananchi wa Makusi kuwa wavumilivu katika kipindi hiki na utaratibu ukikamilika soko litajengwa


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo