Mzee wa miaka sabini amwingilia mtoto kimwili Arusha na kumtishia kumuua

Mzee anayekadiliwa kuwa na miaka sabini  mkazi  wa eneo la Unga limited mkoani Arusha anatuhumiwa  kumfanyia vitendo vichafu mtoto  mwenye umri wa miaka kumi  kwa kumwingilia kimwili kwa kipindi kirefu  na kumtishia kumuua endapo atatoa siri hiyo.
Mzee  huyo ambaye ni baba wa kufikia  wa mtoto aliyetendewa kitendo hicho  anadaiwa kusababisha  mtoto huyo kuacha shule na kumkabidhi majukumu mengine ya nyumbani.

Kwa mujibu wa maelezo ya majirani ni kwamba ,kabla ya kubainika kwa kitendo hicho mtoto huyo alianza kushukiwa na majirani wanaomzunguka na baadae walipombana na kutaka awaeleze kinachomsibu ndipo alipowaeleza mkasa mzima huku akimuhusisha mama yake mzazi kuwa kila alipomueleza vitendo anavyofanyiwa na baba yake huyo wa kambo  mama yake  hakuonesha kushtuka.

Nao majirani walioshuhudia tukio hilo  wameonesha kuchukizwa na kitendo hicho  huku wakimshutumu mzee  kutokuwa na ushirikiano na majirani  mtaani hapo  na kudai  kuwa mara kadhaa wamekuwa wakimuhisi kujihusisha na vitendo viovu.

blog hii  ilifika katika shule ya msingi Themi anakosoma mtoto huyo  na kuzungumza na mwalimu mkuu pamoja na mwalimu wake wa darasa na kudai kuwa mtoto huyo aliacha kuja shule kwa muda na walipofuatilia hawakupata majibu na hivyo kutaka kuchukua hatua zaidi ili kujua mwanafunzi huyo yupo wapi.

Kaimu mganga mfawidhi wa hospitali ya mkoa ya  mount Meru Dr Idd Zuberi amesema wamekuwa wakipokea watoto wengi wanaofanyiwa vitendo vya ukatili wa kijinsia  hivyo ameitaka jamii kuwa mlinzi na kuhakikisha kuwa tabia hizo zinakomeshwa.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo