Wanafunzi wavamia mkutano wa mgombea na kumtaka amalize kero ya madawati

Wanafunzi wa shule ya msingi Ibugule Kata ya Khome wilayani Bahi,  wametaka mbunge atakayechaguliwa kuwakilisha jimbo la Bahi, aje na   mkakati utakaowaondolea adha ya kwenda shuleni, wakiwa na mifuko aina  ya salfeti ambayo hutandika chini na kuikalia kufuatia ukosefu wa  madawati.
 
Lucas Samweli (17), anayesoma darasa la sita, Shule ya Msingi  Ibungule, alisema awamu hii ya uchaguzi wanatamani wazazi wao  wawachagulie mbunge, atakayekuwa na ubunifu wa mipango  itakayowaondolea kero, zikiwamo zinazotokana na shule nyingi jimboni  humo kukosa madawati. 
 
Tunawaomba wazazi wetu wasifanye makosa katika kupiga kura, tunataka  watuchagulie viongozi watakaotuondolea kero hii, ambayo mbali na  kusababisha tuchafuke, viungo vya miili yetu vinauma kwa kuandika  tukiwa tumeinamisha migongo ardhini, alisema mwanafunzi huyo.
 
Wanafunzi wapatao watano, walipewa nafasi ya kueleza waliyonayo   mioyoni, katika kipindi hiki cha kuelekea uchaguzi mkuu, kwenye  mkutano wa kampeni za mgombea ubunge wa jimbo hilo kupitia Chama Cha  ACT Wazalendo, Eva Kaka.
 
Kaka kwa nyakati tofauti alifanya mikutano ya kampeni katika vijiji  vya Ibugule na Khome, katika Jimbo la Bahi, mkoani Dodoma.
 
Alisema matokeo mabaya yanayoonekana katika matokeo ya mitihani  mbalimbali wanayofaya, ikiwamo ile ya kumaliza elimu ya msingi ambayo  ni mitihani ya kitaifa, kiini ni mazingira mabaya ya kusomea. 
 
Alisema ingekuwa amefikia umri wa kupiga kura, angechunguza ahadi  zinazotolewa na kila mgombea udiwani na kuzilinganisha na maelezo  yaliyoandikwa kwenye ilani ya chama chake, ili kujiridhisha kuwa  mtazamo na msimamo wa chama cha mgombea husika, anayo dhamira ya  kweli katika kutekeleza majukumu hayo.

Chanzo:Nipashe 


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo