Wanafunzi wa Shule za Msingi Kisiwa kilichopo Ukerewe Mwanza wanasoma kwa zamu kutokana na ukosefu wa madarasa.
“Hali ya Wanafunzi kupata elimu ni jambo la msingi lakini miundombinu hairidhishi, shule yetu ina majengo mawili yenye vyumba vine vya madarasa, wanafunzi wanasoma kwa zamu”—Mwenyekiti wa Kitongoji, Muzumari Kasanzila.
Mwenyekiti huyo amesema Diwani wa Kata yao amehamia Morogoro na MbungeSalvatory Machemuli hajafika muda mrefu kisiwani hapo hivyo hajui matatizo ya Wananchi wake.