Na Rahim Sakabona, Kyela.
Timu ya soka iliyo chini ya umri wa miaka 15 Kyela House Academy Sport Club yenye maskani yake hapo wilayani Kyela juma mosi hii ya tarehe 22/8/2015 inategemea kusafiri mpaka Katumba Songwe kukipiga na Katumba Academy.
Mchezo huo ni wakirafiki wenye lengo la kukuza viwango vya soka kwa watoto hapa wilayani Kyela umategema kuanza majira ya saa 10:30 za jioni katika uwanja wa Shule ya msingi Katumba.
Kocha mkuu wa Kyela House Academy Maiko Funga Mwango, amesema vijana wake wamejipanga vizuri kuhakikisha wanaibuka na ushindi katika mchezo huo.