ALIYEKUWA DC MAKETE APONGEZA POSHO ZA VIKAO VYA SENSA KUFUTWA

Wananchi wilayani Makete wametakiwa kutoa ushirikiano kwa kushiriki kikamilifu katika sensa ya watu na makazi inayotarajiwa kufanyika nchi nzima Agosti 26 mwaka huu

Hayo yamesemwa na aliyekuwa mwenyekiti wa kamati ya sensa na mkuu wa wilaya ya Makete Mh. Zainabu Kwikwega wakati wa kikao cha wajumbe wa kamati hiyo kilichofanyika katika ukumbi wa halmashauri ya wilaya ya Makete

Amesema pamoja na hayo pia anaipongeza hatua iliyofikiwa na serikali kwa kufuta posho za vikao vya sensa nchi nzima kutokana na uhaba wa fedha na kuwataka watu wote wanaotakiwa kufanikisha zoezi hilo kufanya kazi zao kwa moyo na bila kinyongo ili zoezi hilo lifanikiwe

Katika kikao hicho wajumbe walijadili changamoto mbalimbali zinazolikabili zoezi hilo pamoja na namna ya kutatua changamoto hizo, ikiwa ni pamoja na kuwashirikisha wanahabari, viongozi wa dini, asasi zisizo za kiserikali pamoja na wadau mbalimbali ili kufanikisha kufikisha elimu kwa jamii


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo