LHRC yaitaka serikali kutoa machapisho ya kutosha ya katiba pendekezwa

Wakati taifa likielekea kuipigia kura katiba inayopendekezwa kumejitokeza changamoto  ya upatikanaji wa  katiba hiyo kutokana na kuwepo na machapisho machache ya katiba inayopendekezwa na hivyo kituo cha sheria na haki za binadamu(LHRC) kimeitaka serikali kuchapisha  machapisho ya kutosha ya katiba hiyo ili wananchi waweze kuisoma na kuielewa.
Hayo yameelezwa na mwanasheria wa kituo cha sheria na haki za binadamu (LHRC) Bi.Geline Fuko wakati akizungumza katika mikutano mbalimbali ya kutoa elimu kuhusiana na katiba inayopendekezwa  mjini songea.
 
Bi.Geline Fuko amesema katika maeneo mbalimbali waliyozunguka wamebaini kuwa  machapisho ya katiba  pendekezwa  yako machache hivyo wameitaka serikali  kuchapisha machapisho hayo ya kutosha.
 
Katika mkutano uliofanyika chuo cha ualimu Songea TTC na kuwashirikisha wanachuo na walimu katika chuo hicho wanachuo wamekosoa katiba pendekezwa  kutokidhi matakwa ya wananchi.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo