Jeshi la polisi linawashikilia watu watatu kwa makosa ya kuwakuta na karatasi 860 za dola bandia mkoani Ruvuma

Jeshi la polisi mkoani Ruvuma linawashikilia watu watatu akiwemo  mzambia mmoja kwa kukutwa na karatasi  nyeusi 860 za dola bandia za kimarekani zikiwa katika mafungu ya bunda kumi ambapo kila bunda lina karatasi themanini na sita huku pia wakiwa na malighafi ya kutengeneza dola hizo ambazo wakichanganya na karatasi hizo zinageuka kuwa dola bandia.

Kamanda wa polisi wa mkoa wa ruvuma ACP MIHAYO MSIKHELA amewataja watuhumiwa wa tukio hilo kuwa ni Boniface   Simwanza mwenye miaka 41 raia wa zambia,Adamu Msongore mwenye miaka 26 mkazi wa tunduma mkoani mbeya na Hatman Steven mkazi wa makumbusho Songea huku pia wakiwa na malighafi za kutengeneza dola bandia.
 
Kamanda Msikhela amesema kuwa polisi inaendelea na uchunguzi wa tukio hilo na utakapokamilika watuhumiwa watafikishwa mahakamani kujibu tuhuma za tukio hilo. 

Kufuatia tukio hilo jeshi la polisi mkoa wa Ruvuma linawataka wananchi hasa wafanyabiashara kuwa waangalifu na matapeli wanaotengeneza noti bandia 


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo