MWANAMKE HUYU AOLEWA MARA MBILI....MUME WA PILI HAKUJUA KITU...!!!

Rings-on-FingersIshu ni kwamba kuna mwanaume alikutana na msichana wakapeana namba za simu wakawa wanawasiliana, wakaanzisha uhusiano, baadae wakafunga ndoa.. kilichoibuka baadae kumbe yule mwanamke ni mke wa mtu !!
Mwanaume huyo amesema alipokutana na mwanamke huyo alimwambia kuwa ni mwanafunzi  wa kidato cha tatu, wakaendelea na uhusiano hadi binti alipomueleza kuwa amemaliza shule na kujiunga VETA, akasoma mpaka akamaliza. uhusiano wao ulidumu kwa miaka miwili, hakuna tatizo lolote lilitokea hapo katikati.
Wakakubaliana waoane.. Mwanaume akapeleka barua ya posa kwa wazazi wake na harusi ikafungwa nyumbani kwao Zanzibar.
Wakiwa ukumbini wazazi wa mwanaume wakasikia tetesi kuwa mwanamke huyo ameolewa na ana familia yake.. wakaanza kufuatilia na kugundua kuwa mwanamke huyo ameolewa na ana watoto wanne, yuko kwenye ndoa kwa miaka 16.. ndoa hii mpya haikwenda mbali, ilivunjika ndani ya wiki moja.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo