Kiganja cha mtoto Baraka Cosmas mwenye ulemavu wa ngozi kilichokatwa Machi 8 kwenye kijiji cha Kipeta Sumbawanga kimepatikana mwishoni mwa wiki Wilayani Mbozi.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya Ahmed Msangi alisema kiganja hicho kilipatikana kutoka kwa mkazi wa kijiji cha Malonje Sajenti Kalinga ambaye anafanya kazi ya Useremala.
Alisema awali walimkamata mganga mganga wa kupiga ramli ambaye ndiye aliyehusika kukata kiganja hicho na baada ya kumbana Mganga huyo alimtaja Kalinga ndiye aliyemtuma kuleta kiganja hicho cha albino.
“Tulimbana mtuhumiwa akatuambia aliyemtuma ni Kalinga kwa dau la milioni 100″Msangi.
“Polisi walifika kwa mtuhumiwa Kalinga na walipomuhoji kwa kina alikitoa kiganja hicho na kuwakabidhi”
Hadi juzi watu sita walishikiliwa kwa tuhuma za kuhusika na tukio hilo wakiwemo waliokamatwa mwaka jana na wengine mwaka huu.
