WATENDAJI WA SERIKALI WATAKAOSHINDWA KUWALINDA ALBINO KUKIONA CHA MTEMA KUNI

 Serikali imesema haitasita kuwachukulia hatiua za kisheria watendaji wa vijiji,kata, wilaya na mkoa watakao shindwa kudhibiti mauaji ya walemavu wa ngozi kwenye maeneo yao na kuwataka wananchi  kutowachagua wanasiasa wanaojihusisha na imani potofu za kishirikina ili kupungumza mauaji ya kinyama yanayotia doa nchi ya tanzania katika mataifa yanayoendelea duniani.

Changamoto hiyo imetolewa jijini mwanza katika mkutano wa hadhara ulioitishwa na kamati ya amani ya viongozi wa dini mkoa wa mwanza kwa lengo la kulaani mauaji ya walemavu wa ngozi albino yaliyoibuka kwa staili ya kuteka nyara watoto chini ya umri wa miaka mitano ambapo mkutano huo umehudhuriwa na maelfu ya wananchi kutoka mikoa ya kanda ya ziwa, wanasiasa, viongozi wa dini, watendaji wa serikali, wafanyabia shara wakubwa kwa wadogo,wasomi kutoka vyuo vya elimu ya juu na wasanii maarufu hapa nchini ambapo waziri mkuu wa Tanzania alialikwa kama mgeni rasmi na kuwakilishwa na waziri wa nchi uratibu na uhusiano katika ofisi ya rais Mh.Mary Nagu ambaye amesema kuwa serikali haitavumilia unyama unaotendeka kwa jamii.
 
Kwa upande wake mkuu wa mkoa wa mwanza Bw.Magesa Mulongo amewataka wakuu wa wilaya kuwakamata watuhumiwa bila huruma yoyote na kwamba atakayebainika ameshindwa kutimiza wajibu wake atachukuliwa hatua za kisheria ikiwa ni pamoja na kuachishwa kazi ili kutekeleza kauli mbiu ya mkoa wa mwanza juu ya walemavu wa ngozi inayosema tunaishi pamoja,tunakula pamoja,tunacheza pamoja katika nchi moja
 
Katika kongamano hilo  wananchi kwa pamoja wamejitolea kuchangia fedha chama cha walemavu wa ngozi mkoa wa mwanza ambapo zaidi ya shilingi milioni sita zimepatikana huku wananchi wakichangia kiasi cha shilingi milioni moja,waziri wa nchi uratibu na uhusiano katika ofisi ya rais Mh.Mary Nagu amechangia kiasi cha shilingi milioni moja na mfanyabiashara maarufu jijini mwanza Bw.All Taf Dogo Mansoor ametoa shilingi milioni nne  ambapo viongozi wa chama cha walemavu wa ngozi mkoa wa mwanza wameiomba jamii iwathamini kwa kuwalinda.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo