Chadema yaitaka NEC kuongeza vifaa zoezi la uandikishaji wapigakura

Chama cha demokrasia na maendeleo (CHADEMA),kimeitaka serikali kuiongezea tume ya taifa ya uchaguzi (NEC), vifaa vya kutosha na muda ili kufanikisha zoezi la uandikishaji wa wapigakura kwa mfumo wa BIOMETRIC VOTERS’ REGISTRATION – BVR, ili kuhakikisha kila mtanzania mwenye sifa ya kupiga kura anaandikishwa kwa ajili ya uchaguzi mkuu ujao.

Akifungua mkutano wa kamati tendaji kanda ya ziwa victoria, baraza la uongozi wa kanda hiyo inayoundwa na mikoa ya kagera, geita na mwanza pamoja na wadau, mwenyekiti wa chadema taifa Mh. Freeman Mbowe ameitaka serikali kuipatia tume ya taifa ya uchaguzi fedha za kutosha ili zoezi linaloendelea la kuandikisha wapigakura kwenye daftari la kudumu liweze kufanikiwa, ambapo amesema tume hiyo hadi sasa imepokea mashine 80 tu za BVR kati ya 800 zinazohitajika nchi nzima.
 
Akizungumzia mauaji ya watu wenye ulemavu wa ngozi na vikongwe yanayoendelea kutokea katika mikoa ya kanda ya ziwa kwa imani za ushirikina na tamaa ya baadhi ya watu kujipatia utajiri wa haraka haraka, ambapo hadi sasa inakadiriwa kuwa watu 76 wenye UALBINISM wamekwisha uawa hapa nchini tangu mauaji hayo yalipoibuka, mwenyekiti huyo wa chama cha demokrasia na maendeleo amesema jambo hilo linapaswa kukomeshwa na serikali kwa nguvu zote na watuhumiwa kufikishwa mbele ya vyombo vya dola.
 
Akimkaribisha kufungua mkutano huo wa siku mbili, naibu katibu mkuu wa chadema – Zanzibar Salum Mwalimu amesema ni jambo la kusitikisha kuona serikali ikijivunia kuzindua kivuko kipya cha MV. DAR ES SALAAM kitakachosafirisha abiria kati ya Dar es salaam na Bagamoyo na kutumia saa nne kwa maelezo kwamba kitasaidia kupunguza msongamano na foleni.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo