SIMBA YAIPONGEZA YANGA KWA USHINDI WAKE MNONO DHIDI YA WAZIMBABWE

Simba wametoa pongezi kwa watani wao wa jadi Yanga kutokana na ushindi wa mabao 5-1 dhidi ya FC Platinum ya Zimbabwe.


Yanga imeshinda kwa mabao  hayo na kujiweka katika nafasi nzuri katika michuano ya Kombe la Shirikisho Afrika.
Mjumbe wa Kamati ya Utendaji ya Simba, Said Tully amesema kwa niaba ya Rais wa Simba, Evans Aveva wanaipongeza Yanga.

“Yanga ni wawakilishi wa nchi katika michuano ya kimataifa. Hakika wanastahili pongezi kutokana na kufanya vema.

“Inapofikia katika suala la nchi, si vibaya kuwapongeza. Tukirudi kwenye ligi basi upinzani unaendelea.

“Ndiyo maana leo tulikuwa uwanjani kushuhudia Yanga wakipambana na walifanya vema kwa kweli,” alisema Tully.

Yanga imeitandika FC Plutinum kwa mabao hayo matano katika mechi nzuri ya kuvutia kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo