Serikali mkoani Kilimanjaro, imetoa saa
48 kwa maofisa watendaji kata, vijiji na mitaa, kufanya zoezi maalum la
uhakiki wa wageni, wanaodaiwa kutumia mwavuli wa dini kuendesha biashara
haramu ya wizi wa watoto.
Agizo hilo limekuja siku chache baada ya
kugundulika mahali walipofichwa watoto 29, wanaodaiwa kupotea kwenye
mazingira ya kutatanisha katika mikoa 13 nchini na kuhifadhiwa kwenye
makazi hayo kinyume cha sheria za nchi.
Mkuu wa mkoa huo, Leonidas Gama
alisema unalenga kusaidia kupunguza hofu na hasira ya umma kuhusiana na
usalama wa watoto hao; na mahali wanakopelekwa baada ya kupatiwa
mafunzo maalum ya kujihami pamoja na elimu ya dini.
โNimeagiza
ndani ya saa 48, kila mtendaji kwenye ngazi za vijiji, mitaa na kata,
wawe wamewatambua watu wote na kuwasilisha taarifa za siri kwa wakuu wa
wilaya zao. Baada ya zoezi hilo nitatoa taarifa rasmi kwa umma, Jumanne
ya wiki ijayo kuhusu hali ya usalama katika mkoa wetu,โ Gama.
Watoto walio okolewa hadi sasa, baada ya
kugunduliwa kwa matukio hayo ni wenye umri wa miaka miwili hadi 16,
ambao walikutwa wamehifadhiwa kwenye nyumba moja, iliyopo karibu na
uwanja wa Mandela, Kata ya Pasua, Manispaa ya Moshi, mali ya
mfanyabiashara wa nguo nchini Kenya, Abdelnasir Abdurahaman, maarufu
kama Karata (33), huku watoto wengine 11, wakiokolewa pia katika kituo
cha UMM Sakhail, kilichopo Lyamungo, Wilaya ya Hai.
Hata hivyo, kwa mujibu wa Tangazo la
Serikali namba 280 la mwaka 2002, pamoja na kifungu cha 353 cha Sheria
ya Elimu, iliyofanyiwa marejeo mwaka 2002; mzazi yeyote au mlezi
atakayeshindwa kuhakikisha mwanae anapata elimu ya msingi kwa wakati
husika, atashtakiwa, kulipishwa faini au kupata adhabu ya kifungo, iwapo
atashindwa kutimiza matakwa ya sheria hiyo.
Kufuatia taharuki hiyo kuikumba mikoa ya
Kilimanjaro, Arusha na Manyara, Mkuu wa Jeshi la Polisi Nchini (IGP),
Ernest Mangu, juzi alilazimika kukutana na kutetea kwa zaidi ya saa sita
na timu ya makachero wa makao makuu ya jeshi hilo pamoja na maofisa
wake wa mkoa wa Kilimanjaro, ikiwa ni siku tano baada ya kukamatwa kwa
wafanyabiashara wanaodaiwa kuwahifadhi watoto kutoka mikoa mbalimbali
nchini.
Alipoulizwa iwapo watoto hao, wanatokea mikoa ipi ya Tanzania; Kamanda wa Polisi mkoani hapa, Geofrey Kamwela,
alisema uchunguzi wa awali unaonyesha kuwa watoto hao ni wakazi wa
mikoa ya Tanga, Mtwara, Mbeya, Tabora, Manyara, Arusha, Kagera, Mara,
Kilimanjaro, Dodoma na Shinyanga.