CHOMBO MAALUM CHENYE NGUVU YA KUSHUGHULIKIA DAWA ZA KULEVYA KUUNDWA

Na Christina Mwagala
 
KUFUATIA kuwepo kwa baadhi ya viongozi  wengi wa serikali na dini  kujihusisha na biashara ya dawa za kulevya Serikali imedhamiria kuunda chombo chenye nguvu kwa ajili ya kupambana nao.
 
Akizungumza katika maadhimisho ya siku ya kupambana na madawa ya kulevya nchini yaliyofanyika leo katika viwanja vya shule ya msingi Tandale jijini Dar es Salaam, Waziri wa mambo ya ndani Dk Emanuel Nchimbi, alisema biashara ya dawa za kulevya isipodhibitiwa ipasavyo kuna hatari ya nchi kushindwa kuongozwa
 
Nchimbi aliyemuwakilsha waziri mkuu alisema athari za dawa za kulevya zinaathiri sekta zote pasipo kujali utashi wa mtu, na kwamba wanaoathirika zaidi ni vijana ambao ni nguvu kazi ya Taifa.
 
Alisema kuwa tabia yawatu kujihusisha na biashara haramu yadawa zakulevya inazidi kuota mizizi hapa nchini kutokana na tamaa ya viongozi kutaka kupata utajiri wa haraka bila kujali kuwa inaleta madhara makubwa kwa wanachi.
 
Aliongeza kuwa Serikali imejipanga kukabiliana na tatizo hili nah ivyo hadai sasa tayari imeanza  kuanzisha mchakato wakuhakikisha kuwa serikali inapata chombo  chenye nguvu kiutendaji cha kupambana na dawa za kulevya ambacho kitanzishwa hivi karibuni nakuanza kazi maramoja.
 
Nchimbi aliongeza kuwa tatizo la dawa za kulevya bado lipo hapa nchini na linazidi kukua kila mwaka na hivyo  Serikali   kupitia vyombo vya ulinzi na usalama vinatakiwa kujikita katika kupambana na biashara hizo ilikuhakikisha kuwa tatizo hili linakwisha kabisa.
 
Nchimbi alisema zao la bangi limezidi kuwa tatizo zaidi kutokana na kupatikana kirahisi kutokana kuzao hilo kulimwa kwa wingi katika mikoa iliyo athirika ikiwemo  Tanga, Mbeya na Iringa. Nahivyo kuagiza kamati  za ulinzi na usalama za mikoa yote hapa nchini kuhakikisha zinasimamia na kuratibu udhibiti wa kilimo hiki na kuwasaidia wananchi ili waweze kushiriki katika kilimo cha mawazo mbadala.
 
Madhara ya dawa za kulevya yamekuwa yakikusababisha mfumuko wa bei za bidhaa mbalimbali na hivyo kuleta ugumu wa maisha kwa wananchi,huku akilituhumukupoea kwa nguvu kazi yataifa siku hadisiku.
 
Nchimbi alisema kuwa  watumiaji wadazakulevya wamekuwa nikeroi kubwa kutokana na vijana wengi kupata Magonjwa mbalimbali yamambukizi yakiwemo ukimwi  na homa ya ini hali inayopelekea wengiwao kupoteza maisha.
 
Aidha aliongeza kuwa nchi inaweza kuingia vitani kutokana na biashara haramu ya dawa za kulevya kama ilivyotokea nchini Colombia na vurugu za magenge yanayojihusisha na biashara hiyo haramu zinazoendelea hivi sasa nchini Mexico na hivyo kama nchi yetu haitakuwa makini kwa kuwashugulikia   viongozi wa kisiasa waliojiingiza kwenye biashara hizo itajikuta inakuwa kama hizo.
 
“Nchi inapokuwa kitovu cha biashara haramu ya dawa za kulevya inajivunjia hadhi ya kimataifa na wananchi wake hushukiwa kila wanaposafiri nje ya nchi, hupata tabu sana katika viwanja vya ndege vya kigeni pindi wanaposafiri kwa kushukiwa na kupekuliwa sana. kwa wale watanzania ambao wanajihusisha na biashara hii nje ya nchi watambue kwamba adhabu kali za vifo zita wakabili kama hawata jirekebisha”alisema nchimbi.
 
Hata hivyo Nchimbi amekiri kuwepo kwa tatizo lar ushwa  katika  kudhibiti watumiaji wa madawa ya kulevya miongoni mwa watendaji wa serikali amabapo alisema kuwa wapo baadhi ya watendaji ambao si waadilifu katika utendaji kazi wa kila siku haliinayo sababisha kurudisha nyuma  jitihada za serikali kupiga vita tatizo hilo.
 
Kaulimbiu ya mwaka huu ni tujenge jamii yenye afya bila Dawa za kulevya,na tutoe maoni yakatiba nakushiriki sensa.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo