Mwili wa marehemu Kepten John Komba umewasili rasmi mjini Songea tayari kwa mazishi hii leo

Mwili wa marehemu Kepten John Komba aliyekua mbunge wa jimbo la Mbinga Magharibi mkoani Ruvuma, umewasili rasmi mjini Songea jana tayari kwa mazishi yatakayofanyika kijijini kwake Lituhi wilaya ya Nyasa na kuongozwa na rais Mh. Jakaya Kikwete hapo kesho majira ya mchana.

Ni majira ya saa 10:30 jioni, mwili wa marehemu Kepten John Komba ukawasili katika uwanja wa ndege mjini Songea ukiambatana na familia ya marehemu, viongozi mbalimbali akiwemo katibu wa bunge, na wabunge wote wa mkoa wa Ruvuma ambapo mapokezi hayo yameongozwa na mkuu wa mkoa wa Ruvuma, Said Mwambungu.
 
Na baadaye mwili wa Kepten John Komba ukapelekwa katika uwanja wa majimaji mjini Songea, ambapo maelfu ya wakazi wa Songea wakiwa hawaamini kilichotokea na kushikwa na simanzi kubwa wamejitokeza kuuaga mwili wake huku foleni ikiashiria wazi kwamba siyo wote watakaofanikiwa kuuona mwili wa Kepten Komba kwa mara ya mwisho.
 
Mwili wa marehemu Kepten John Komba unatarajiwa kuzikwa Leo kijijini kwake lituhi wilaya ya nyasa ambapo mazishi yake yataongozwa na rais Mh. Jakaya Kikwete.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo