Baada
ya kutemwa na CHADEMA, Zitto Kabwe aenda jimboni kwake Kigoma Kaskazini
kuzungumza na wananchi wake.
Mbunge wa Kigoma Kaskazini Zitto Kabwe
amewataka wakazi wa Kigoma kutosikitishwa na mambo yanayomkabili kwa
sasa ila wamuunge mkono kwa hatua yoyote atakayoichukua kwa kuwa ni
wanasisasa wengi wamepitia katika misukosuko kama yake.
Zitto ametoa kauli hiyo Kigoma alipokutana na viongozi 250 wa vijiji Kigoma alipokutana nao LEO.
“Msinililie mimi kwa kuwa haya ni mapito
ya kila mwanasiasa makini, wengi walitofautiana na vyama vyao kwa
sababu ya ya maslahi ya mataifa yao.. hivyo jukumu kubwa ni kuniunga
mkono…”
Mbunge huyo amesema hadi sasa hajapewa
taarifa yoyote ya kusitishwa kwa Ubunge wake, lolote likitokea atarudi
kuwafahamisha juu ya uamuzi wake.
