Rapa
King Crazy GK ambae jana ametambulisha wimbo wake mpya unaokwenda kwa
jina la 'Shukrani' amefunguka na kusema kuwa wimbo huo ameutoa maalumu
kwa ajiri ya kuwashukuru wadau mbalimbali na mashabiki ambao walikuwa
wakimsubiri wakati wote
AY/GK/Mwana FA
akiwa
masomoni na pia kuwashukuru wasaniii ambao wamepigania kuutangaza na
kuufikisha mbali zaidi muziki ukilinganisha na kipindi ambacho wao
walikuwa wakifanya muziki.
GK alisema kuwa huu ni kama mwanzo wa mashabulizi hivyo ameona bora
kushukuru kwanza kabla ya kazi rasmi kuanza,kwa mujibu wa Gk alisema
kuwa baada ya hiii kazi tutegemee kusikia kazi kutoka katika kundi la
Muziki wa Hip Hop ambalo lilifanya vizuri miaka ya nyuma East Coast Team
ambalo liliundwa na wakali kama Ay,Mwana FA,Buff G,Soud Brouwn,Oten
pamoja na amiri jeshi mwenyewe King Crazy GK.
"Wimbo huu nimetoa kwa ajiri ya kuwashukuru wadau wa muziki,mashabiki
wangu pamoja na wasanii wenzangu kama kina Vanessa Mdee,Diamond Platnum
ambao wameweza kuufikisha muziki mbali zaidi na kupata tuzo mbalimbali
nje ya Tanzania,hii inaonyesha wazi kuwa muziki wetu kwa sasa umekuwa
hivyo kuna tofauti na miaka ile sisi tunafanya muziki,Mshabiki wategemee
kuisikia ile East Coast Team ya zamani maana mpaka sasa kuna kazi tatu
zishafanyika na ziko tayari ila tunafanya kuchagua kazi ipi iwe ya
kwanza kutoka baada ya hii Shukrani ya kwangu"
Mbali na hili King Crazy GK emeelezea sababu kubwa ya kufanya kazi
hii na Vanessa na kusema kuwa aliangalia kwa sasa msanii gani anaweza
kusikilizwa na watu wote katika jamiii ndipo alipogundua kuwa Vanessa
anaweza kufikisha ujumbe kwa watoto,vijana na hata watu wazima na ndio
maana alimua kufanya nae hiyo kazi.