DKT. SLAA APELEKA MALALAMIKO YA KUTAKA KUUAWA NA MLINZI WAKE MAKAO MAKUU YA POLISI DAR

KATIBU Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Dk. Wilbroad Slaa (pichani kushoto) muda huu ametoka katika ofisi za Makao Makuu ya Polisi jijini Dar es Salaam alipokwenda kupeleka malalamiko yake ya kutaka kuuawa na mlinzi wake aitwaye Khalid Kangezi.
 
Dk. Slaa amekabidhi malalamiko yake hayo kwa maandishi ambapo zaidi ya kurasa tisa amezikabidhi kituoni hapo.

Akiongea na wanahabari, Dk. Slaa amesema kuwa hajaitwa na mtu yeyote kituoni hapo kuhojiwa kama ilivyodhaniwa hapo awali bali ameenda mwenyewe kwa ajili ya kukabidhi malalamiko yake.

Dk. Slaa amekaa ofisini hapo kwa zaidi ya saa tano ambapo waandishi wa habari walizuiliwa kuingia ndani hivyo kulazimika kusubiri nje ya ofisi hiyo hadi alipomaliza kuandika malalamiko yake.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo