TAARIFA KUHUSU MBUNGE NIMROD MKONO KUTEKWA NA WATU WASIOJULIKANA

Kwa mujibu wa gazeti la mtanzania Mbunge wa Musoma vijijini Nimrod Mkono wa CCM amenusurika kutekwa na watu wasiojulikana katika eneo la Tanki bovu jijini Dar es salaam.

“Nikiwa na msaidizi wangu tukitoka Bagamoyo tukiwa ndani ya gari langu aina ya Marcerdez Benz katika eneo la Tank bovu gafla yalitokea magari mawili na kutuziba kwa mbele lakini dereva baada ya kuona hali iyo aliondoa gari kwa kasi akipita pembeni na kufainikiwa kutoka eneo hilo”alisema Mkono.

Alisema baada ya kutoka eneo hilo magari hayo aligeuza na kumfuata yakiwa mwendo kasi na baada ya kuwafikia kijana mmoja aliyekua amevaa miwani nyeusi alishusha kioo na kututaka tusimamishe gari.

“Dereva wangu aliondoa tena gari kwa kasi hadi njia panda ya Kawe ambapo tulimkuta askari wa zamu na kumwelezea na kuomba msaada wake na baada ya muda kidogo magari hayo yaliwapita kwa kasi eneo hilo yakielekea Mbezi Beach na askari yule alitushauri kwenda kutoa taarifa kituo cha polisi”alisema.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo