ALIYEKUWA mnenguaji na mwimbaji wa Bendi ya Twanga Pepeta, Aisha
Madinda aliyefariki jana asubuhi, atazikwa kesho mchana badala ya leo
kama ilivyokuwa imepangwa hapo awali.
Mtoto wa kwanza marehemu, Feisal amesema kuwa polisi wamesema ni
lazima mwili wa mama yake ufanyiwe upasuaji (postmortem) ili kujua
chanzo cha kifo chake.
Awali ndugu wa marehemu walisema hawahitaji Asha Madinda afanyiwe
upasuaji, lakini baada ya polisi kutembelea eneo la tukio la kifo chake
huko Mabibo, wamesema ni lazima upasuaji ufanyike.
Feisal amesema upasuaji unatarajiwa kufanyika leo mchana hali
inayowalazimisha kubadili ratiba ya mazishi. Aisha Madinda sasa atazikwa
kesho mchana baada ya sala ya Ijumaa.
(HABARI: SAIDI MDOE)