Mtu mmoja amewafyatulia risasi watu
wawili na kupelekea mmoja kufariki na mwingine kujeruhiwa akiwalalamikia
kumpigia kelele wakati watu hao walipokuwa kwenye mkesha wa harusi Dar.
Mkuu wa Upelelezi Mkoa wa Kipolisi
Ilala, David Mwambunga amethibitisha kutokea kwa tukio hilo japo
amekataa kuzungumzia suala hilo kwa kuwa yeye sio msemaji rasmi.
Majeruhi wa tukio hilo, Goodluck
Madaraka amesema siku ya tukio walikuwa wakicheza muziki majira ya saa
tano usiku ndipo jirani yao Lucas Muhabe alitoka na panga akiwafukuza
kwamba wanampigia kelele, muda mfupi baadaye akarudi na bastola na
kuanza kupiga risasi hewani ambapo moja ilimpata mpita njia Mahamudu
Muhasi kichwani, akafariki.
Kaka wa marehemu amesema mdogo wake alikuwa akipita njia tu jirani na ilipo sherehe hiyo hivyo ameuawa lakini hakuhusika.
