Kamanda wa Polisi Mkoa wa Ilala Mary
Nzuki amesema wanamshikilia mfanyabiashara Lucas Sasha kwa kosa la
kumuua mpita njia Mahmoud Ally kwa kumpiga risasi maeneo ya Tabata
Kisukulu wakati wa sherehe za Christmas.
Kwa mujibu wa maelezo aliyoyatoa Sasha
amesema kuwa kulikuwa na kundi kubwa la vijana waliokuwa wanapita mbele
ya nyumba yake hivyo akadhani kuwa amevamiwa na vibaka, akaamua kupiga
risasi.
Kamanda Nzuki amesema mfanyabiashara
huyo anamiliki bastola hiyo kihalali, kwa sasa Polisi wanamshikilia kwa
ajili ya uchunguzi wa tukio hilo
JIUNGE NA EDMO BLOG SASA
Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube
Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi