ASHIKILIWA NA POLISI BAADA YA KUMUUA MPITA NJIA KWA KUMPIGA RISASI

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Ilala Mary Nzuki amesema wanamshikilia mfanyabiashara Lucas Sasha kwa kosa la kumuua mpita njia Mahmoud Ally kwa kumpiga risasi maeneo ya Tabata Kisukulu wakati wa sherehe za Christmas.

Kwa mujibu wa maelezo aliyoyatoa Sasha amesema kuwa kulikuwa na kundi kubwa la vijana waliokuwa wanapita mbele ya nyumba yake hivyo akadhani kuwa amevamiwa na vibaka, akaamua kupiga risasi.

Kamanda Nzuki amesema mfanyabiashara huyo anamiliki bastola hiyo kihalali, kwa sasa Polisi wanamshikilia kwa ajili ya uchunguzi wa tukio hilo


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo