ANGALIA JINSI MVUA ZILIVYOLETA MADHARA HUKO SINGIDA

 Zaidi ya nyumba hamsini na moja zinazo kadiriwa kuwa na wakazi zaidi ya miambili, katika Manispaa ya Singida, zimebomolewa na Mvua kubwa ya mawe iliyonyesha ikiambatana na upepo mkali.
 
Mvua hiyo iliyoanza kunyesha majira ya jioni imesababisha hasara kubwa kwa wakazi wa manispaa hiyo ambapo, mpaka sasa nyumba hamsini na moja zimeharibiwa ikiwemo Nyumba za watu binafsi na Madarasa ya Misikiti.

Mkuu wa Wilaya Qeen Mlozi amesema …”Serikali ya Mkoa kwa kweli mvua iliyonyesha jana takribani dakika kumi na tano paka ishirini ilikuwa mvua kubwa ya mawe na upepo mkal,  ambayo imesababisha  nyumba nyingi za mjini Singida zimeharibiwa na upepo, paka sasa wakati wataalam wanaendelea jumla ya nyumba hamsini na moja , zimeanguka, zimeharibiwa, zimeezuliwa na upepo”

Ally Sanga Mkazi wa Singida amesema… “Imekuja mvua tuu mida ya jioni hii imedumu kama dakika 15 hivi alafu umekuja upepo mkali na mawe, ndio imesababisha madhara yote ambayo mnayaona imeangusha Nyumba, Miti, Nyaya za umeme zimekatika yani watu wana hali mbaya sana”

Wakazi wa Manispaa hiyo wamesema Mvua iliyonyesha haijawahi kutokea pamoja na kunyesha kwa muda mfupi, lakini imeleta madhara makubwa sana na kulalamikia Manispaa ya Singida kwa kutokutengeneza vizuri miundombinu ya maji na kusababisha Nyumba nyingi kubomoka.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo