MALERIA YAUA MMOJA KATI YA WAHAMIAJI HARAMU WALIOKAMATWA MKOANI PWANI



Mmoja wa raia wa Ethiopia waliokamatwa kwenye msitu wilayani Bagamoyo wakituhumiwa kuwa wahamiaji haramu na kulazwa hospitalini kutokana na matatizo ya afya, amefariki akipatiwa matibabu.
 
Dawita Alalo (25) ambaye alikuwa miongoni mwa wahamiaji haramu 11 waliolazwa kwenye kituo cha afya cha Chalinze, wilayani Bagamoyo,  alifariki juzi  kwa ugonjwa wa malaria.
 
Kaimu Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Pwani, Athuman Mwambalaswa alisema Alalo alikuwa miongoni mwa raia 48 wa nchi hiyo walioingia nchini isivyo halali.
 
Walikamatwa Agosti 22 mwaka huu  wakiwa kwenye msitu wa Kijiji cha Visakazi Ubena Zomozi tarafa ya Chalinze.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo