BASI LA HOOD LAGONGANA NA BASI LA ISAMILO MKOANI ARUSHA

Watu mia moja na ishirini wamenusurika kifo na wengine kujeruhiwa katika eneo la Kikatiti wilayani Arumeeru baada ya mabasi ya Hood lililokuwa linatoka Arusha kwenda Iringa kugongana na basi la Isamilo lililokuwa linatoka Moshi kuelekea mkoani  Mwanza.

Wakizungumza baada ya kutokea ajali hiyo baadhi ya mashuda na abiria waliyokuwemo katika ajali hiyo  wamesema dereva wa basi la Hood alikuwa katika saiti yake lakini ghafla lilitokea basi la Isamilo lililokuwa linalipita Lori la mizigo kwenye kona  kali pamoja na daraja ndipo likashinda na kuingia upande wa pili.


Kwa upande wake dereva wa basi la Hood ambaye pia ameumia mkono katika ajali hiyo amesema basi alililogongana nalo likuwa kwenye mwendo kasi ambao ulimshinda dereva kulimudu gari hilo huku alitoa wito kwa madereva wengine kuwa makini wanapo kuwa bara barani .

Akizungumza kwa njia ya simu kamanda wa polisi mkoa wa Arusha Lebaratus Sabas amethibitisha kutokea kwa ajali hiyo.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo