WALAJI WA MBOGA ZA MAJANI NCHINI HATARINI KUKUMBWA NA KANSA YA UTUMBO

Walaji wa mboga za majani zisizo salama wapo hatarini kukumbwa na magonjwa ya kansa ya utumbo na homa ya matumbo kutokana na mazingira hatari ya uoteshaji, na baadhi ya wakulima kutumia madawa pasipo kufuata utaratibu kwa lengo la kuzalisha mboga hizo kwa wingi. 

Katika jicho letu mikoani Waandishi wetu Mariam Adams,Projestus Binamungu na Silivester Bulengala wametuandalia taarifa inayojikita katika hatari za matumizi ya mbogo za majani zisizo salama. 

Huu ni moja ya mfereji wa maji machafu ambayo hutililika kutoka katika viwanda na makazi ya watu jijini Mwanza.

Pembezoni mwa mfereji huu shuguli za kilimo cha mboga mboga zinafanyika na maji haya ndio haswa hutumika katika umwagiliziaji.

Wataalamu wa afya hushauri ulaji wa mboga za majani kama moja wapo ya kiungo muhimu katika kukamilisha mlo kamili. 

Mazingira yanayotumika katika uandaaji na utunzaji wa bustani kwa baadhi ya sehemu bado ni hatari licha ya wakulima kunyosheana vidole. 

Mbali na wakulima ambao hutumia maji kutoka vyanzo visivyo salama,kwa wakulima ambao wanaendesha kilimo cha mbogamboga cha kisasa baadhi yao wanahusishwa na matumizi holela ya dawa kwa malengo ya kujinufaisha kifedha. 

Mbali na changamoto hizo kiafya, kilimo cha mboga za majani ni nguzo kuu kwa baadhi ya wajasiriamali hususani akina mama katika kujikwamua na umasikini.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo