Na Sweetbert Lukonge na Hans Mloli
MWENYEKITI wa Kamati ya Uchaguzi ya Simba SC, Damas Ndumbaro, amesema wazi kuwa aliyekuwa mgombea wa nafasi ya urais klabuni hapo, Michael Wambura, alifoji barua iliyoonyesha kuwa amerudishiwa uanachama wake.
MWENYEKITI wa Kamati ya Uchaguzi ya Simba SC, Damas Ndumbaro, amesema wazi kuwa aliyekuwa mgombea wa nafasi ya urais klabuni hapo, Michael Wambura, alifoji barua iliyoonyesha kuwa amerudishiwa uanachama wake.
Hatua hiyo inakuja baada ya Wambura kuwasilisha barua tatu
zilizoonyesha aliwahi kusimamishwa na uongozi wa Simba, kisha ukamsamehe
zikiwa kama ushahidi wa kujitetea na mapingamizi aliyowekewa katika
uchaguzi wa Simba unaotarajia kufanyika Juni 29, mwaka huu ambapo sasa
imegundulika kuwa kiongozi huyo alidanganya.
Imeelezwa kuwa Wambura alisimamishwa uanachama wake Simba baada ya kuipeleka klabu hiyo mahakamani mwaka 2010.
Akizungumza na waandishi wa habari jana Jumapili kwenye Makao Makuu
ya Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) jijini Dar, Ndumbaro alisema barua
aliyoiwasilisha Wambura kuwa alisamehewa, imefojiwa kwa kuwa Katibu Mkuu
wa Simba wakati huo, Evodius Mtawala amekana kutia saini ya barua hiyo.
“Moja ya barua zile tatu zilizoonekana zina utata, ile ya mwisho ya Septemba 25, 2012 iliyoonyesha kuwa Wambura amesamehewa inaonekana dhahiri imefojiwa kwa sababu tumemuuliza Mtawala na amesema hii si saini yake iliyopo kwenye hii barua.
“Kwa hiyo utaona moja kwa moja kuwa barua hii Wambura aliifoji na
wala haikuwa halali kutoka Simba na hili ni kosa kisheria,” alisema
Ndumbaro ambaye ni Mwanasheria kitaaluma.
Mei 25, mwaka huu ambayo ilikuwa ni siku ya wagombea kujibu mapingamizi yao, Wambura aliwasilisha barua tatu zinazomwonyesha kuwa yeye ni mwanachama halali baada ya kusamehewa kutokana na kuipeleka Simba mahakamani lakini baadaye zilileta mkanganyiko kutokana na kupishana kwa tarehe za maombi na majibu.