TUHUMA ZA UFISADI ZAIBUKA TENA BUNGENI KUHUSU WIZARA YA NISHATI NA MADINI

Wabunge wa bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wamelaani vitendo vya kifisadi vinavyoendelea kwenye baadhi ya taasisi za Wizara ya Nishati na Madini na kulitaka bunge kuunda Kamati teule ya kuchunguza wa ufisadi wa Shilingi bilioni 200 kwenye akaunti inayojulikana kwa jina la Escrow fedha ambazo zinadaiwa kupotea kwenye mazingira ya kutatanisha.

akaunti hiyo ilifunguliwa kufuatia mgogoro baina ya Kampuni ya kufua umeme ya IPTL na Tanesco ambapo Shirika hilo la Umeme nchini lilipaswa kuilipa Kampuni ya IPTL kupitia akaunti hiyo hadi hapo mgogoro huo utakapomalizika ambapo fedha hizo zinadaiwa kupotea kinyemela.

Kwa upande wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini inasema kuna haja ya fedha za miradi kutolewa kwa wakati ili kusaidia upatikanaji wa uhakika wa nishati ya umeme nchini.

Awali akiwasilisha bajeti hiyo Waziri mwenye dhamana Profesa Sospeter Muhongo anasema bado kuna fikra potofu kuwa serikali haijawawezesha watanzania kuwekeza kwenye sekta ya madini.

Wizara ya Nishati na Madini imeomba kuidhinishiwa jumla ya Shilingi Trioni 1, bilioni 82 katika mwaka mpya wa fedha 2014/2015 ambapo miongoni mwa fedha hizo Shilingi Bilioni 957.1 sawa na asilimia 88.4 ya bajeti hiyo kutumika kwenye miradi ya maendeleo huku Shilingi Bilioni 125.3 sawa na asilimia 11.6 kwajili ya matumizi ya kawaida


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright 2025 EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo