Sakata la kuwaondoa wafanyabiashara katika maeneo yao ya kufanyiabiakazi mjini njombe limendelea kushika kasi licha ya bunge kuzuia wafanyabia katika sehemu mbalimbali za miji mpaka serikali Itakapo tenga maeneo kwaajili ya kufanyia shughuli zao.
Hali hiyo
imejitokea Mapema leo baada ya wafanyabiashara wanaofanyia biashara zao
katika Maeneo mbalimbali Likiwemo eneo la Roman Catholiki Mjini Njombe
kujikuta katika wakati mgumu baada ya uongozi wa kata ya njombe mjini
kwa kushirikiana na uongozi wa mitaa mbalimbali kuambatana na Askari
Polisi na Migambo Kwa lengo la Kutaka Kuwaondoa Katika Maeneo Hayo.
Zoezi
hilo Limekuwa likifanyika mara kwa mara lakini wafanyabiashara hao
wamekuwa wakishindwa kutekeleza agizo la kuwataka wahame katika eneo
hilo ambalo ni hatari kwa usalama wao kutokana na kushinda pembezoni mwa
barabara kuu ya Njombe Songea wakijishughulisha na ujasiliamali kwa
kuuza vitu mbalimbali.
sakata hilo leo Imeonekana kuwa tishio kwa
wafanyabiashara hao ambao wamesema Serikali imekuwa ikiwalazimisha
kuhama katika maeneo hayo ilihali hakuna maeneo shirikishi katika
masuala ya kibiashara wanakooneshwa.
Kutokana na Hali Hiyo Kituo
hiki kimelazimika kuwatafuta baadhi ya viongozi wa ngazi ya mitaa na
kata ili kutolea ufafanuzi huo ambao Afisa mtendaji wa Kata ya Njombe
Mjini Bwana Bonasius Mwalongo Amesema Kuwa Kama Serikali Haiwezi
kuwaacha katika Maeneo Hayo Waendelea kufanya biashara hizo kwani ni
hatari katika maisha yao na wateja wao.
Bryson Lupenza ni Afisa
mtendaji wa Mitaa ya Kwivaha,National Housing na Mgendala,Mitaa ambayo
imekuwa katika sakata hilo Ambaye Amesema Kuwa Amekuwa Akitoa Elimu kwa
Wafanyabiashara Hao Zaidi ya mara 20 Lakini Wamekuwa Wakishindwa kutii
Agizo la kuhama Katika Maeneo Hayo.
Agrey Mtambo ni Diwani wa Kata
ya Njombe Mjini Ambaye Amesema Kuwa Bado Hajapokea Malalamiko hayo
Lakini Ataendelea Kushughulikia Kwani Serikali inawajibu wa Kuwahamisha
taratibu Mara baada ya kuwaandalia Maeneo Rafiki Katika Biashara Zao.
Wakati
Bunge la Bajeti likipitisha Makisio ya Bajeti Katika Wizara ya Viwanda
na Biashara Liliitaka Serikali Kuwaacha Wafanyabiashara Hao hadi pale
Serikali Itakapo watengea Maeneo ya Kazi Hiyo Lakini Bado Azimio Hilo
Limeonekana Kuendelea Kukiukwa na Baadhi ya Viongozi wa Mitaa na Kata.