KLABU YA YANGA YAPATA MSIBA WA ALIYEWAHI KUWA MWENYEKITI WAKE

ALIYEWAHI kuwa Katibu Mkuu wa Dar es salaam Young Africans George Johnson Mpondela ‘Castor’ amefariki dunia jana saa nne usiku katika hospitali ya Muhimbili, Dar es Salaam alikokuwa amelazwa kwa matibabu ya moyo.

Mtoto wa Marehemu Bwana Hilton amesema kwamba baba yake aliyekuwa akiishi eneo la Machava, Kigamboni, Dar es Salaam amekuwa akisumbuliwa na maradhi ya moyo kwa miaka minne sasa.

Amesema msiba uko nyumbani kwao, eneo la Karakata, Uwanja wa Ndege karibu na Kanisa Katoliki na kituo kidogo cha Polisi, maarufu Polisi Posti.

Marehemu ameacha mke na watoto tisa, ambao ni Pius, Robert, Hilton, Kennedy, Joseph, Collin, na wa kike Linda, Jaqcueline na Jennifer.

Hilton amesema mwili wa marehemu utasafirishwa Jumanne kwenda Tabora baada ya kuagwa kuanzia Saa 2:00 asubuhi hospitali ya Muhimbili tayari kwa mazishi yake Jumatano kijiji cha Misha wilaya ya Tabora vijijini.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo